Na Jumia Food Tanzania
Kutokana na mabadiliko
ya namna tunavyoishi hivi sasa suala la afya limekuwa ni jambo la msingi ambalo
watu wengi wanalizingatia. Magonjwa yanayotokana na mienendo ya mifumo ya
maisha watu wanayoishi sasa yamekuwa yakikua kwa kasi kiasi kwamba kampeni za afya
zimekuwa zikishika hatamu kila kukicha.
Ukiachana na mazoezi au
kupunguza kula aina fulani ya vyakula ili kuufanya mwili wako uwe wenye afya na
kujikinga na baadhi ya maradhi, kuna baadhi ya tabia ambazo ukizianza sasa
zinaweza kuwa na manufaa makubwa kwako. Jumia
Food imekukusanyia faida 6 ambazo unaweza kuzipata
kutokana na kuanza kunywa maji yenye limao kila unapoianza siku yako.
Inasaidia mmeng’enyo wa
chakula. Asidi zilizomo kwenye tumbo husaidia kuvunjavunja
chakula tunachokula ili kumeng’enyeka kwa urahisi. Na kwa kunywa maji yenye
limao asubuhi kunaweza kusaidia kuongeza asidi tumboni, ambazo hupungua kadri
umri wetu unavyoongezeka.
Inasaidia mwili kuwa na
maji. Maji hupotea mwilini kwa njia nyingi zikiwemo
kutoka jasho, kukojoa, kutapika, kuharisha na kadhalika. Na kutokana na
miongoni mwetu kuwa na mfumo wenye pilikapilka nyingi za kutafuta kipato, wengi
huwa hatunywi maji ya kutosha kitu ambacho siyo kizuri kwa afya ya miili yetu.
Hivyo basi, kwa kunywa maji yenye limao asubuhi husaidia mwili wako kuwa na
maji.
Husaidia kuzuia mawe
kwenye figo. Hii hutokana na mabaki
ya madini na chumvi kwenye figo yanayojikusanya na kuwa vitu vigumu mfano wa
mawe. Mojawapo ya sababu inayopelekea hali hii ni upungufu wa maji mwilini. Na
uwepo wake mwilini huwa na madhara kama vile damu kwenye mkojo, maumivu wakati
wa kukojoa nakadhalika. Hivyo, kwa kunywa maji yenye limao kila siku asubuhi
kunaweza kusaidia kuzuia kutokea kwa mawe hayo kwenye figo mwilini.
Huupatia mwili potasiamu
inayohitajika. Haya ni madini muhimu
ambayo mwili yanayahitaji ili uweze kufanya kazi ipasavyo. Potasiamu ni muhimu
kwa mawasiliano ya mishipa ya misuli na kusafirisha virutubisho na taka mwili.
Kwa kunywa maji yenye limao kila asubuhi kutasaidia mwili kupata potasiamu
inayoihitaji.
Yana vitamini C ya
kutosha. Kunywa maji yenye limao kila asubuhi kusaidia
mwili kuupatia virutubisho vyenye vitamini C inayoihitaji, ambayo ni muhimu
katika kulinda kuharibika kwa seli na kupona majeraha.
Husaidia kupunguza uzito
wa mwili. Mbali na kuachana na tabia za kula aina za
vyakula fulani au kufanya mazoezi ili kukusaidia kupunguza uzito wa mwili, pia
kunywa maji yenye limao kila asubuhi ni tiba mbadala.
Zipo faida nyingi za
kuanza kunywa maji yenye limao ambazo Jumia Food haiwezi kuziorodhesha zote
hapa kama vile kusaidia kupunguza harufu mbaya ya kinywa. Faida mojawapo kwa
watanzania wengi ni kwamba malimao yanapatikana kwa urahisi, gharama nafuu na
takribani kipindi chote cha mwaka. Anza sasa kutumia limao kama tiba mbadala
kwa afya ya mwili wako, naamini utaratibu huu utakuwa ni wenye manufaa kwako.
Comments
Post a Comment