Na Jumia Travel Tanzania
Kutokana
 na maendeleo ya sayansi na teknolojia binadamu waliyonayo kwa sasa si 
jambo la kushangaza kumuwezesha mtu akafanya shughuli zako zote akiwa 
yupo sehemu moja ndanin ya muda mfupi.
Kwa
 mfano, kwa kutumia simu yako ya mkononi unaweza kutatua changamoto 
kadhaa hapo nyumbani kwako kama vile kufanya miamala ya fedha kutoka 
benki na kisha kutoa kwa mawakala huduma za fedha, kulipia umeme, 
kulipia maji, kulipia king’amuzi, kuagiza chakula, kuagiza usafiri, 
kufanya manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali.
Lakini
 swali ni kwamba, je ni watanzania wangapi wanaiona fursa hiyo 
iliyoletwa na teknolojia kama suluhu za changamoto tofauti 
zinazowazunguka?
Jibu
 ni kwamba ni watu wachache sana walioyapokea maendeleo yaliyoletwa na 
teknolojia na kuyatumia katika kurahisisha maisha yao ya kila siku. Ni 
jambo la ajabu kuona kwamba mtu ameishiwa na umeme nyumbani kwake lakini
 hana suluhu yoyote zaidi ya kwenda kwa mawakala wa huduma za malipo 
wakati yeye mwenyewe anao uwezo wa kufanya hivyo kwa kutumia simu yake 
ya mkononi.
Zipo
 sababu kadha wa kadha zinazopelekea watu wengi kushindwa kuzitumia 
huduma hizi ipasavyo mojawapo ikiwa ni elimu ya kuweza kuitumia mifumo 
na programu hizo. Ila kwenye suala la elimu sidhani kama ni hoja ya 
msingi kwa sababu mifumo takribani yote ni rahisi kwa mtumiaji na 
kikubwa zaidi ni kwamba ukiwa unaitumia mara kwa mara inazoeleka kwani 
hakuna kinachobadilika.
Kampuni ya Jumia
 ambayo imejikita kwenye masuala ya biashara kwa njia ya mtandao barani 
Afrika katika nyanja za hoteli na usafiri, manunuzi ya bidhaa, kazi, 
makazi, magari, chakula na matangazo mbalimbali imetimiza miaka mitano 
(5) tangu kuanzishwa kwake.
Katika
 maadhimisho ya sherehe hizo kampuni hiyo imekuwa ikifanya mikutano kwa 
njia ya ‘video za moja kwa moja’ na wataalamu na waasisi wa makampuni 
mbalimbali ya kiteknolojia duniani. Lengo kubwa likiwa ni kupata 
ushauri, uzoefu na mitazamo juu ya ukuaji wa sekta hiyo na mustakabali 
wake barani Afrika.
Mojawapo
 ya wageni walioalikwa kwenye mfululizo wa ‘video’ hizo alikuwa ni Afisa
 Mtendaji Mkuu na mwasisi mwenza wa Andela, Bw. Jeremy Johnson ambayo ni
 kampuni iliyoanzishwa kwa madhumuni makubwa ya kuwafunda watengeneza 
program barani Afrika (Softwarfe Developers) na kisha kuwaunganisha na 
makampuni yenye uhitaji wa wataalamu hao. Mpaka hivi sasa Andela 
imefungua matawi yake katika nchi tatu ambazo ni Nigeria (Lagos), Kenya 
(Nairobi) na mapema mwaka huu waliongeza tawi lingine jijini Kampala, 
Uganda.
Bw.
 Johnson katika mazungumzo yake na wafanyakazi wa Jumia alieleza kwamba 
mojawapo ya vigezo wanavyoviangalia mpaka wanafikia hatua ya kufungua 
tawi nchi husika ni baada ya kufanya utafiti wa kutosha wa maendeleo ya 
teknolojia pamoja na shauku ya wananchi wa eneo husika katika kuitumia 
ili kutatua changamoto mbalimbali za maisha yao ya kila siku.
Hoja ya msingi iliyoainishwa na mwasisi huyo ambayo Jumia Travel
 imeibaini katika mazungumzo yake ni utayari na shauku ya watu kutumia 
teknolojia. Kwa hoja hiyo kwa haraka haraka tunaweza kuona kwamba nchi 
za Nigeria na majirani zetu wa Kenya wametuacha hatua kadhaa katika 
kuyapokea mabadiliko ya kiteknolojia na kuyatumia ipasavyo. Na suala 
hilo ni mojawapo ya sababu zinazopelekea makampuni kadhaa kuanzia katika
 nchi hizo kabla ya kuvuka mpaka na kuja nchi nyingine ikiwemo Tanzania.
Imefikia
 mahali sasa watanzania kubadilika na kuyapokea mabadiliko yanayoletwa 
na teknolojia hususani mtandao wa intaneti katika kurahisha maisha yetu 
ya kila siku. Zipo huduma nyingi ambazo unaweza ukazipata kwa kubonyeza 
tu vitufe vya simu yako mahali popote ulipo na ukazipata. Tukumbuke 
kwamba mabadiliko haya yote huja kwa malengo ya kufanya shughuli zetu 
ziwe rahisi tofauti na awali na ndiyo maana watu wanaendelea kufanya 
uvumbuzi kila kukicha.  

Comments
Post a Comment